Header Ads

Kiharusi (stroke) ni nini? Na tiba yake ni nini?

STROKE NI UGONJWA GANI?
Skull with red to indicate stroke
Strokes occur due to problems with the blood supply to the brain; either the blood supply is blocked or a blood vessel within the brain ruptures.
Stroke Ni Nini?

Stroke au kiharusi ni tatizo linalotokea ghafla kwenye ubongo ambapo mtiririko wa damu kwenye eneo fulani la ubongo husitishwa ghafla au kupungua sana hivyo kusababisha eneo hilo la ubongo kukosa damu na virutubisho muhimu na seli za eneo hilo kuanza kufa. Hili linaweza kutokea pale mishipa ya damu ya kuelekea kwenye eneo hilo ikiziba au mishipa ndani ya ubongo katika eneo hilo kupasuka. Seli za ubongo za eneo hilo zikianza kufa kwa kukosa damu, shughuli zote zinazoendeshwa na eneo hilo la ubongo husimama kwa mfano kumbukumbu au misuli. Kiharusi ni ugonjwa wa dharura hivyo tiba inatakiwa ipatikane mapema iwezekanavyo. Kimsingi kiharusi huweza kumpata mtu ye yote wakati wo wote.
Kuna aina tatu za stroke; ischemic, hemorrhagic na TIA. Kundi la watu lililo kwenye hatari kubwa zaidi ya kuupata ugonjwa huu ni lile la watu wenye miili mikubwa, umri zaidi ya miaka 55, wenye historia ya ugonjwa huu kwenye familia zao, ambao hawafanyi mazoezi , wanaokunywa sana pombe au kutumia madawa haramu.

Kiharusi Husababishwa Na Nini?    
   
Kila moja ya aina za stroke hapo juu inasababishwa na vitu tofauti.
Ischemic strokes, ndiyo aina ya stroke inayowaathiri watu wengi zaidi, asilimia 85 ya wagonjwa wa stroke hupatwa na aina hii ya stroke. Aina hii ya stroke husababishwa na kuziba kwa arteri (mishipa ya kusafirisha damu safi) zinazoelekea kwenye ubongo au kusinyaa kwa mishipa hiyo hivyo kusababisha hali inayoitwa ischemia (upungufu mkubwa wa mtiririko wa damu).


Kuziba kwa mishipa ya damu hutokea baada ya damu kuganda ndani ya arteri zinazoeleka kwenye ubongo au katika maeneo ya mbali zaidi na kusukumwa kwenye mishipa yenye kipenyo kidogo ndani ya ubongo. Mishipa hii inaweza kuzibwa pia na mafuta yaliyoganda ndani ya arteri (plaque).
Hemorrhagic strokes, husababishwa na arteri ndani ya ubongo kuvuja damu au kupasuka. Damu hii iliyovuja huleta mgandamizo kwenye seli za ubongo na kuziharibu. Kupasuka kwa mishipa ya damu husababishwa na hypertension, trauma au dawa zinazofanya mishipa hii ya damu kupungua unene wake.


Transient ischemic attack (TIA), hii ni tofauti na aina hizo mbili za stroke hapo juu kwani hapa mtiririko wa damu kuelekea kwenye ubongo huvurugwa kwa muda mfupi kwa sababu zile zile tulizozitaja hapo juu tulipozungumzia ischemic strokes. Stroke ya aina hii ni ishara ya kutokea strokes nyingine baadaye kama hatua zinazostahili hazitachukuliwa.

Dalili Za Kiharusi (Stroke)

Ugonjwa wa stroke humpata mtu ghafla na dalili hutokea kwa muda mfupi sana.
 Dalili kuu za ugonjwa huu ni:
 Kuchanganyikiwa, mtu akipata shida ya kuongea na kuelewa            anachoambiwa
Maumivu ya kichwa yanakwenda pamoja na kupoteza fahamu kwa vipindi na kutapika
Ganzi katika viungo vya uso, mkono na mguu na hasa vikiwa vya     upande mmoja wa mwili
Kupana shida ya kuona kwa jicho moja au yote
Kupata shida ya kutembea vikichanganyika na kizunguzungu na     kukosa mpangilio wa matendo ya mwili

Athari za kiharusi zinaweza kuwa ni za muda mrefu. Kulingana na muda uliopita kabla ya kuugundua na kuutibu ugonjwa huu, mtu anaweza kupata ulemavu wa muda mfupi au wa kudumu. Pamoja na madhara ya stroke kama yalivyoorodheshwa hapo juu, mgonjwa wa stroke anaweza pia kupata yafuatayo:
 Msongo wa mawazi
Maumivu kwenye mikono na miguu yanayoongozeka baada ya       viungo hivyo kufanya kazi au kutokea mabadiliko ya hali ya hewa.Kupooza au udhaifu wa upande mmoja wa mwili
Kupata shida katika kufanya matendo ya kuonyesha hisia za mwili
Kushindwa kumudu matumizi ya kibofu cha mkojo au viungo vya njia ya haja kubwa
  Dalili zingine za kiharusi au stroke ni:
Kupoteza fahamu kwa ghafla kwa kipindi fulani cha muda
Kupooza ama kupata Udhaifu wa mwili upande mmoja,ama
Wakati mwingine,pande zote za mwili hupooza.
Kupoteza uwezo wa kuona kwa ghafla kwa kipindi fulani
Kupoteza uwezo wa kuongea ama kushindwa kuumba maneno vizuri
Kupata ganzi na kuhisi vitu vinakuchomachoma mikononi na miguuni
Kuchanganyikiwa ghafla(confusion) kwa muda
Kukosa balance ya kutembea ama kushindwa kabisa kutembea
Kichwa kuuma sana unahisi kama kinapasuka ikiambatana na kutapika(hili huwa halitokei sana kwa wengi).


Tiba Za Stroke Na Namna Ya Kuzuia Stroke

Kwa vile aina kuu mbili za stroke, ischemic na hemorrhagic, kila moja ina chanzo kilicho tofauti, kila moja inahitaji tiba iliyo tafauti na ya aina nyingine. Ni shurti kujua kwa uhakika ni aina gani ya stroke iliyotambuliwa kwani tiba ya stroke ya aina moja inaweza kuwa na madhara kwa stroke ya aina nyingine.
Tiba kwa Ischemic Stroke: Ischemic strokes hutokea pale mishipa ya damu inapoziba au kupungua kipenyo hivyo tiba ya tatizo hili ni kuhakikisha damu ya kutosha inaufikia ubongo. Tiba huanza kwa kotoa dawa za kuyeyusha damu au mafuta yaliyoganda na kuzuia hali hiyo isitokee tena. Aspirin yaweza kutumika au sindano ya tissue plasminogen activator (TPA).
Tiba kwa Hemorrhagic stroke: Stroke ya aina hii hutokea pale damu inapovuja ndani ya ubongo hivyo tiba yake italenga katika kuzuia damu isiendelee kuvuja na kupunguza mgandamizo wa damu iliyovuja kwenye ubongo. Tiba huanza kwa kutoa dawa za kupunguza mgandamizo kwenye ubongo, kupunguza msukumo wa damu kwa ujumla na kuzuia kusinyaa kwa ghafla kwa mishipa ya damu. Upasuaji unaweza kutumika kurekebisha mishipa ya damu iliyopasuka .
Ili kujilinda na stroke au kuzuia stroke yafuatayo yanaweza kufanywa:
Kutotumia madawa haramu
Kula chakula chenye mboga na matunda kwa wingi na chenye         cholesterol kidogo
Kufanya mazoezi kila wakati Kuhakikisha unadhibiti blood pressure
Kuhakikisha unadhibiti kiwango cha sukari mwilini
Kuwa una uzito unaofaa
Kunywa pombe kwa kadri au kuacha kabisa
Kuacha kuvuta sigara


No comments

Powered by Blogger.