Header Ads

Yatambue magonjwa /maradhi yanayotibika kwa kutumia tu kitunguu saumu (Garlic),(vallium sativum)





Kitunguu saumu ni nini?

Kitunguu swaumu ni jamii ya vitunguu ambayo kwa kitaalamu huitwa Allium sativum

Kitunguu saumu kina baadhi ya muunganiko wa vitu vifatavyo

1.Protini
2.Chumvi chumvi
3.Viua saumu
4.Vimengenyo
5.Homoni na n.k....







Magonjwa yanayotibika kwa kutumia /faida /kazi za kitunguu saumu

BAADHI YA MARADHI/MAGONJWA YANAYOTIBIWA NA KITUNGUU SWAUMU;
1.Kiua sumu
2.Kisafisha tumbo
3.Kiyeyusha mafuta(cholestro)
4.Huzuia mvilio wa damu
5.Kusafisha njia ya mkojo
6.Kutibu amoeba
7.Kuzuia kuhara damu(Dysentery)
8.Tumbo kushindwa kumeng'enya(Indigestion)




9.Gesi kujaa tumboni
10.Msokoto wa tumbo
11.Typhoid
12.Kidonda kilichooza
13.Dondakoo
14.Mabaka
15.Baridi yabisi(Rheumatisim)
16.Mishipa
17.Uziwi
18.Virusi vya homa ya mafua(Influenza)
19.Mafua
20.Saratani(Cancer)
21.Kifaduro
22.Kifua kikuu cha mapafu
23.Kipindupindu
24.Kutoa minyoo
25.Upele
26.Kuvunjavunja mawe katika figo




27.Mba kichwani
28.Kuupa nguvu ubongo
29.Kuupa nguvu fizi
30.Kuzuia meno kung'ooka
31.Nguvu za kiume
32.Maumivu ya kichwa
33.Kizunguzungu/kisunzi
34.Kutuliza maumivu ya meno
35.Kujenga misuli na kutia nguvu
36.Mkakamo wa ateri(Arteriosclerosis)
37.Shinikizo la damu
38.Kinga ya tauni na ukimwi
39.Magonjwa ya macho
40.Hurekebisha homoni kwa wanawake wenye  mvurugiko wa homoni

Yafatayo ni baadhi ya maelezo kuhusu matumizi na namna kitunguu saumu kinavyo Fanya kazi 

KITUNGUU SAUMU
kimekuwa kikitumika kutibu na kuboresha afya ya mwili na hivyo kumfanya mtumiaji awe mrembo na mwenye afya bora.




Matumizi ya kitunguu saumu kibichi yamekuwa yakisaidia vitu vingi sana mwilini.

Baadhi ya hayo ni pamoja na kupambana na virusi, bakteria, fangasi na pia sumu mbalimbali hasa zile zinazosababishwa na baadhi ya vyakula mwilini.

Kutokana na hilo, matumizi ya kitunguu saumu kama tiba na kipodozi, ni jambo linalopendekezwa na wataalamu wa urembo wa asili.
Katika matumizi yake kitunguu saumu hutumika kwa kula na wakati mwingine kupaka, ambapo hili hutegemea zaidi na mahitaji au matatizo ya mtumiaji husika.

Pamoja na njia hizo nilizotaja hapo juu, lakini wataalamu wanashauri ulaji wa kitunguu saumu kibichi kila siku, kwani husaidia kuboresha afya ya muhusika.

Ikiwa utashindwa kukitafuna chenyewe, unaweza kuchanganya kwenye chakula kingine ambacho unatumia alimradi tu ukipate kikiwa halisi.
Kwenye urembo, kitunguu saumu husaidia kuondoa matatizo yafuatayo;
Chunusi

Changanya kitunguu saumu kilichosagwa kijiko kimoja na kijiko kimoja cha juisi ya ndimu. Chukua pamba na paka sehemu zote zilizoathirika. Kaa na mchangyiko huo kwa muda wa dakika 15 hadi nusu saa.Ikiwa utaendelea kwa muda wa wiki moja. Tatizo la chunusi litakuwa limeondoka kabisa.





Kunyonyoka kwa nywele
Ni kwa muda mrefu sasa kitunguu saumu kimekuwa kikitumika kama tiba ya kunyonyoka kwa nywele. Unachotakiwa kufanya ni kutumia mafuta yake kwa kupakaa kwenye ngozi ya kichwa kila siku kabla ya kulala. 
Fanya hivyo mara kwa mara kwa muda usiopungua miezi mitatu na utaona matokeo yake. Ikiwa utakosa mafuta yake, si vibaya ikiwa utatumia kitunguu chenyewe kilichosagwa kwa kupaka kwenye ngozi ya kichwa kila siku usiku na kuosha asubuhi yake.

Fangasi vidoleni
Kupambana na fangasi kwenye vidole vya miguu na mikono, unashauriwa kutumia kitunguu saumu kilichosagwa kwa kupaka eneo lililoathirika. Hakikisha unakaa nacho usiku kucha ukiwa umevaa soksi ama glavu. Fanya hivyo kila siku hadi utakapoona muwasho na maumivu yameisha.

MBA
Paka kitunguu saumu kilichosagwa katika ngozi ya kichwa ama sehemu yeyote iliyoathirika. Hakikisha unatumia hadi pale ugonjwa utakapokuwa umetoweka kabisa.

MATUMIZI KATIKA NCHIMBALIMBALI:
kitunguu ni kiambatanisho muhimu kidishi kimaendeleo katika sehemu nyingi ulimwenguni.
Zamani Egpta iliheshimiwa kuwa ya hadhi ya kimungu.

MAANDALIZI YA KITUNGUU SAUMU KIMADAWA:
Kitunguu saumu na asali. Jaza chupa ya glasi na vitunguu saumu vilivyomenywa na
kukatwa katwa polepole mwaga katika asali ya kwamba inajaza nyufa katikati ya fundo ya

kitunguu. Weka glasi kwenye sehemu ya joto yenye c 20oc. Katika siku mbili hadi wiki nne,
asali itanyonya juisi ya kitunguu saumu na kitunguu hicho kitachechemea na kutoingiza

mwanga usichuje. Tumia katika muda wa miezi 3.
Kitunguu Saumu dawa ya kikohozi

Ponda kijiko cha chai cha kitunguu saumu katika kipimo hicho hicho cha sukari au asali.
Tumia mara moja k.mf. kwa kikohozi.
Kitunguu saumu mafuta. Weka g 200 za vitunguu vilivyokobolewa saga kitunguu saumu na

kuweka kwenye chombo cha glasi na ongeza mafuta ya kutosha (au vizuri mafuta ya chakula)





funga. Funga jagi kwa kubana vizuri, na weka ikae kwenye sehemu yenye joto kama C 20
kwa siku tatu. Tikisa mara chache kila siku. Halafu weka kwenye sehemu ya baridi, bila

kuchuja. Tumia katika muda wa mwezi mmoja.
Kitunguu saumu „tinkcha“. Loweka g 200 za vitunguu vilivyomenywa na kukatwakatwa
katika lita moja ya brandi au alikoholi 40-50%, kwa siku 14 kwenye C 20° katika chupa

yenye kufungwa vizuri bila kupitisha hewa. Tikisa chupa hiyo mara nyingi kwa siku. Chuja
vipande vya kitunguu saumu. Tinkcha inakaa muda wa mwaka.

MAPENDEKEZO YA MATUMIZI
Kula kitunguu saumu kibichi- hii ni bora.
Tumia katika kupika.
Kula vitunguu saumu vingi kuzuia magonjwa. Kitunguu saumu ni safi sana kwa mfano kuna
usemi kwamba, chakula chako kiwe ndiyo dawa yako, na dawa yako chakula chako. Hii ni




kweli tu, hata hivyo, kwa kitunguu saumu kibichi, kama ilivyo vitu vingi vyenye nguvu

vinaangamizwa katika kupikwa. Vitunguu saumu vibichi vinatia nguvu katika mfumo wakinga ya maradhi. Matumizi kawaida ya vitunguu saumu yameonyeshwa katika kupunguza
madhara ya magonjwa ya moyo, kiharusi, kansa, msukumo wa damu na homa ya mafua

Makali (flu). 
Tunashauri kwa nguvu ya kuwa wanaoteseka kwa UKIMWI (AIDS) waweke
kitunguu saumu katika chakula chao cha kila siku, kupunguza nguvu ya magonjwa mengine.

Kwa sababu inafanya mara mbili, kwa matumizi ya nje na kwa ndani kama dawa ya kuua
wadudu, vitunguu saumu ni masaada wa kutibu magonjwa yote ya kuambukiza; Toifodi,
minyoo, bilhazia, malaria, damu yenye maambukizo na sumu n.k. Zaidi yake vitunguu saumu

vinaimarisha kumbukumbu, hupunguza shindikizo la damu na Homa, na vinafanya kazi
kupinga ugumu wa kuta za ateri (hardening of arteries). Vitunguu saumu pia vinapinga virusi
na dhidi ya kinyume cha mambo ya fangasi.


1.Majipu au uvimbe na chunjua.




Saga vitunguu saumu vibichi na funga vilivyopondwa kwenye sehemu ya jipu, uvimbe au
Chunjua mara mbili kwa siku na gandamiza. Anza matibabu haya mapema iwezekanavyo.

2. Amiba.
Katakata vitunguu saumu sawasawa vipande vidogo na chukua kijiko kikubwa 1 pamoja na
Chai mara tatu kwa siku (usitafune, kusaidia kupinga kutoa harufu mdomoni). Endelea na
Matibabu haya kwa siku 5. I (H-M Hirt) aliponywa mwenyewe toka Amiba kuharisha
damu kwa Tiba hii.





3. Malaria.
Katakata vitunguu saumu sawasawa. Meza kijiko kimoja cha vitunguu hivi mara tatu kwa
Siku na kunywa lita 2 za limao glasi ya chai kwa siku. Endelea na tiba hii kwa siku 5.
Angalia pia ukurasa wa 8 kwa ajili ya malaria.

4. Kisukari, shindikizo la damu 
kinga ya ugumu wa kuta za arteri (hardening of the
arteries).
Kula vitunguu saumu kwa wingi, vitunguu saumu na vitunguu vinapunguza sukari katika
damu na kusawazisha damu ya cholesteroli, na shindikizo la damu. Badala yake chukua
matone 20 ya vitunguu tinkcha mara 3 kwa siku, basi hii ni pungufu ifuatayo:

5. Kikohozi, homa, sinusitis na kuvimba koo.
a) Kula klovu ya vitunguu saumu mara tatu kwa siku.
b) Chukua kijiko cha chai cha kitunguu saumu asali kila masaa machache.
c) Watoto wanaweza kutumia kijiko cha chai cha kitunguu saumu
mchanganyiko kila baada ya masaa machache.
d) Chukua kijiko cha chai cha kitunguu saumu mafuta mara 6 kwa siku.

6. Kandika.
Chukua kijiko cha chai cha kitunguu saumu au kitunguu saumu yenye asali, kila masaa
machache. Weka mdomoni kwa muda mrefu iwezekanavyo.

7. Fangasi inayoambukiza pamoja na ugonjwa wa ukungu kwenye vidole vya miguu.
Funga sehemu zilizoathirika kwa juisi ya vitunguu saumu vibichi vilivyopondwa au
mafuta.

8. Homa ya matumbo na maambukizo mengine.
Kama itatokea homa ya matumbo, bacillary, kuharisha damu, kifua kikuu, kipindupindu,
trypanosomiasis (ugonjwa wa kusinzia): Siku zote ongeza kitunguu saumu kwa tiba ya
kawaida.

9. Kinga ya mishipa ya damu.
Kitunguu saumu siku zote kinafanya damu kuwa laini na kukinga kutengeneza damu




kuganda ambayo inasababisha shida ya thrombosis. Hii ni muhimu kwa wagonjwa wanaolala kitandani kwa muda mrefu.

10. Kuota meno utotoni.
Futa ufizi kwa fundo la kitunguu Saumu.

Kitunguu thaum kina harufu ya pekee isiyowapendeza watu wengi, ingawa kimebeba siri nyingi za tiba. Kwa ajili hiyo maanayake kwa kilatini ni : harufu ichomayo, na kwa kiarabu lugha ya Quraan huitwa: fuum, nayo ndio sahihi zaidi; kwasababu thaum ni lafdhi ya kihieroglifu ya kifirauni (hieroglyphic).

Allah S.W amesema:
" Na (kumbukeni habari hii kadhalika) Mliposea: Ewe Mussa! hatuwezi kusubiri chakula cha namna moja tu, basi tuombee kwa Mola wako atutolee vile vinavyooteshwa na ardhi kama mboga zake, matango yake, fuum (kitunguu thaum) zake, adesi zake na vitunguu vyake." (2:61)

Iliandikwa katika piramidi (pyramid) huko Misri tangu miaka 4500 iliopita kuwa kitunguu thaum kilikuwa wakipewa wajenzi ya piramidi. Walikuwa wakila kitunguu thaum ili wapate nguvu na nishati.

Mwandishi wa kitabu juu ya tiba zinazotokana na kitunguu thaum alimnasihi mfasiri wake kuwa " Iwapo unataka nguvu, nishati na uwekevu basi kula tembe ya kitunguu thaum na glasi ya maji kila siku kabla ya kula chakula. Daud Al-Antaky ameeleza katika kitabu chake cha Tadhkira kuwa kitunguu thaum hupoza zaidi ya maradhi 40.

Wale wapiganaji wa miereka wa huko Roma walikuwa wakila kitunguu thaum kabla ya kupigana ili wapate nguvu na wepesi.

Imethibitishwa kisayansi kuwa kitunguu thaum husafisha damu kutokana na mafuta (cholestrol) ambayo husababisha magonjwa ya mishipa ya ateri na maradhi ya moyo, na pia husafisha damu kutokana na vijidudu na maikrobati kuliko (antibiotic) vengine. Pia imethibitishwa kwa kuzuia kuenea kwa sumu ya nyoka katika mwili wa mwanaadam na pia husafisha maida kutokana na vimelea (parasites).

Rais wa matabibu, Ibn Sina amesema kuhusu kitunguu thaum: "Kitunguu thaum hulainisha na kuondoa gesi, hutoa vidonda katika ngozi, huhifadhi maji. Vumbi lake likichanganywa na asli akipakwa mwenye ukoma litamfaa, kitunguu thaum humfaa mwenye maradhi magonjwa ya mishipa na nyonga (sciatia). Maji yake (yaliotolewa kwa kupikwa) hutuliza maumivu ya meno, vilevile hufaa kwa kikohozi.

Kitunguu thaum kimekusanya protein 49% mafuta muhimu ya sulphur 25% na kiasi flani cha chumvi, homoni (hormones) zitiazo nguvu za kiume na vinavyoteremsha hedhi.

BAADHI YA MARADHI YANAYOTIBIWA NA KITUNGUU SAUMU:

Kiua Sumu:
Saga tembe tano za kitunguu thaum, changanya na asali kikombe kimoja kilichochanganywa na habbasouda na kunywa papo hapo. Kunywa asubuhi na jioni. Paka mafuta ya kitunguu thaum pahala panapouma iwapo ni sumu ya nyoka au paka nje ya tumbo iwapo umekunywa sumu.

Kusafisha tumbo:
Kabla ya kula chakula, meza tembe za kitunguu thaum na baadae kunywa maji ya shimari yaliyochanganywa na asali kwa muda wa wiki moja.

Kiyeyusha mafuta (Cholestrol):
Unapokula chakula kila siku, weka katika kachumbari kiasi cha tembe 2 vilivyosagwa ule pamoja na kachumbari.

Kiongeza mkojo chenye kusafisha njia za mkojo:
Chemsha vizuri hairi, na baada ya kupoa tia tembe 3 za kitunguu thaum zilizosagwa. Kunywa kinywaji hicho kila siku kabla ya kula na kunywa juisi ya limau/ndimu.

Kuharisha damu (Dysentery):
Chukua tembe ya kitunguu thaum uikatekate na uile; fanya hivyo kwa muda wa wiki moja na bora zaidi ukinywa na mafuta ya zaituni kijiko kimoja.

Gesi na Indegestion:
Kunywa juisi ya pea iliyochanganywa na tembe 3 za kitunguu thaum kabla ya kulala kila siku.

Kutibu Typhoid:
Kata tembe 5 za kitunguu thaum, changanya ndani ya maziwa ya moto yaliyochanganywa na asali kunywa kabla ya kulala. Pia paka uti wa mgongo mafuta ya kitunguu thaum yaliyochanganywa na mafuta ya zeti, na asubuhi vuta moshi wa kitunguu thaum kwa muda wa dakika 5.

Kidonda kilichooza:
Ponda kitunguu thaum mpaka iwe laini kama marhamu halafu jifunge nacho kwa kutumia bendeji, japo kitawasha lakini kitazuia ugonjwa wa gangrene ambao unaweza ukapelekesha kukatwa kiungo. Vilevile unaweza kusafisha kidonda kwa kuchanganya kitunguu thaum kilichosagwa kikatiwa maji vuguvugu (warm water) na kikasafishwa kidonda.

Mishipa:
Kata tembe za kitunguu kitunguu saumu na umeza kwa maziwa ya moto (sio moto sana) yenye matone ya ambari kabla ya kulala kila siku, dawa hii huipa mishipa nguvu.





Homa ya mafua (Influenza):
Kunywa juisi ya machungwa na juisi ya limau zilizochanganywa na tembe 7 za kitunguu thaum kunywa juisi hiyo kabla ya kulala. Vuta moshi wa kitnguu thaum.

Mafua:
Meza tembe za kitunguu thaum baada ya chakula pamoja na juisi ya kitunguu thaum iliyochanganywa na juisi ya limau pamoja na kuvuta moshi wa kitunguu thaum.

Saratani (Cancer):
Katika kitunguu thaum kuna kiini kinachozuia saratani, kwa kila mgonjwa wa saratani anashauriwa ale kwa wingi kitunguu thaum na karoti (carrot).

Kifua kikuu (cha mapafu):
Kila asubuhi kabla ya kula chakula meza tembe 3 za kitunguu thaum, saga ule pamoja na mkate na jioni vuta moshi wake.

Kipindupindu (cholera):
Ili kujikinga na maradhi hayo wakati kikienea, kula kijiko kimoja cha kitunguu thaum kilichosagwa na kukorogewa katika asali baada ya kila chakula.

Kutoa minyoo:
Ponda tembe 3 za kitunguu thaum, tia ndnai ya maziwa na kunywa (bila kutia sukari) jioni kabla ya kulala na asubuhi kunywa mafuta ya mbono.

Upele:
Chukua tembe 5 za vitunguu thaum uvisage na uvikoroge katika shahamu na paka pale penye upele kuazia jioni mpaka asubuhi na ukoshe kwa maji ya moto tumia kwa muda wa wiki moja.





Mbaa kichwani:
Ponda uzuri vitunguu thaum 3 na uvikoroge katika siki ya tofaha (Apple vinegar) katika chupa ya bilauri (sio plastiki) na uache juani kwa muda wa wili moja. Baada ya hapo jipake kichwani pamoja na kusugua kwa muda wa wili 1 na baada ya wiki jipake mafuta ya zeituni.

Nguvu za kiume:
Saga kitunguu thaum kitie ndani ya mafuta ya zeti na weka katika moto mdogo mdogo mpaka iwe rangi ya manjano na tia katika chupa na wakati wa haja jipake katika dhakari na osha baada ya saa moja.

Kujenga misuli na kutia nguvu:
Kila siku kabla ya kula kunywa kikombe kikubwa cha maziwa ya ngamia yaliyotiwa tembe 2 za kitunguu thaum iliyosagwa. Kunywa kwa muda wa mwezi mmoja mfululizo.

Kinga ya taunni na ukimwi:
Ngao kubwa ya maradhi mabaya ni Kumcha Allah S.W mwanzo na mwisho wa siku. Chukua juisi ya kitunguu thaum uichanganye na asali na unywe utafanya hivo pamoja.

KITUNGUU SAUMU. 
tangu kale kimekuwa kikijulikana kama 'dawa ya kushangaza' na kutumiwa na watu wengi katika kutibu mafua na influenza. Miongoni mwa faida za kitunguu swaumu ni kuzuia kupatwa na magonjwa mbalimbali na maambukizo ya virusi. Hivyo kitunguu swaumu hujulikana kama antibiotiki ya asilia. Uchunguzi umeonyesha kwamba kula kitunguu swaumu kunapunguza kushadidi ugonjwa wa influenza na hata kuzuia kupatwa na ugonjwa huo. Vilevile kula kila mara kitunguu swaumu, huzuia kupatwa na magonjwa ya moyo, kwani kitunguu swaumu huzuia damu isigande kwenye mishipa ya damu. 




Halikadhalika kitunguu swaumu ambacho pia ni kiungo muhimu cha chakula kina potassium, na hivyo watu wenye ugonjwa wa shinikizo la damu wanashauriwa kula vyakula vilivyopikwa kwa kitunguu swaumu.
Si vibaya kujua kuwa katika uchunguzi uliochapishwa mwaka 2001, imeelezwa kwamba, kitunguu swaumu kina athari kubwa na nzuri pale kinapochanganywa na baadhi ya dawa nyinginezo katika kutibu Ukimwi au HIV. 
Haya shime jamani… kuanzia leo vyakula visikose kuungwa na kitunguu thomu, iwapo unaogopa kupatwa na influenza kama mimi!
Pia kitunguu saumu kinafanya yafatayo;

  • Vina uwezo wa kusababisha kutanuka kwa mishipa ya damu (vasodilation) kwa kubadilisha polysulfides zilizopo ndani yake kuwa hydrogen sulfides kwenye seli nyekundu za damu.
  • Husaidia uthibiti wa kiwango cha sukari mwilini kwa kushusha kiwango cha kemikali ya homocystine na kupunguza madhara ya kisukari.
  • Iwapo vitapondwa pondwa vizuri, vitunguu saumu hutoa kemikali iitwayo Allicin ambayo ni dawa dhidi ya bateria, na phytoncide ambayo huua fangasi wa aina mbalimbali.


Madhara yasababishwayo na matumizi ya  vitunguu saumu?











Ukiacha faida zake, vitunguu saumu pia vina hasara na madhara mbalimbali kwa mtumiaji. Madhara hayo ni pamoja na;
  • Harufu mbaya mdomoni ambayo hutokana na kemikali ya AMS (allyl methyl sulfide). Harufu mbaya hii, hata hivyo, yaweza kupunguzwa kwa kunywa maziwa au kunywa maji mengi.
  • Kwa baadhi ya watumiaji, vinaweza kuwaletea mzio au mcharuko mwili (allergies au inflammatory reactions)
  • Kichefuchefu, Kutapika na kuharisha.
  • Huweza kusababisha hatari ya kuvuja damu, kwa sababu huzuia kazi ya seli sahani (platelets) zenye kusaidia kuganda kwa damu kushindwa kufanya kazi yake vizuri, na hususani kwa mama wajawazito, baada ya upasuaji au mara baada ya kujifungua.
  • Huingiliana katika utendaji kazi wake na dawa kadhaa kama vile warfarin, antiplatelets, saquinavir, dawa za shinikizo la damu kwa ujumla hasa calcium channel blockers, na antibiotiki za jamii ya quinolone kama vile ciproflaxacillin.





Ahsante

No comments

Powered by Blogger.