Header Ads

Pneumonia

Pneumonia Ni Nini?
Pneumonia ni ugonjwa unaoshambulia vifuko vya hewa kwenye pafu moja au yote mawili. Vifuko hivi huweza kujaa maji au usaha na kusababibisha kikohozi kinachotoa uchafu unaotoka kwenye mapafu, homa na kupata shida katika kupumua.

Vijidudu wa aina nyingi wanaweza kuhusika katika ushambuliaji wa mapafu hayo. Mara nyingi pneumonia hutokana na mashambulizi ya bacteria, virusi, fangasi (fungi) au vijiumbe wengine tegemezi (parasites).

Mtu anapovuta hewa yenye wadudu hawa wadogo (germs) wanaosababisha maradhi, wadudu hawa huingia kwenye mapafu na kama kinga za mwili za mtu huyu zitashindwa kuwazuia, wadudu hawa hukaa kwenye vifuko vidogo (alveoli) vya kwenye mapafu na kuanza kuzaliana.

Mwiliutakapopeleka chembechembe nyeupe za damu kupambana na wadudu hawa, vifuko hivi hujaa majimaji na usaha na kusababisha pneumonia.
     Nini Chanzo Cha Pneumonia

Pneumonia husababishwa na bacteria, virusi, fangasi na vyanzo vingine. Hapa chini tutaona baadhi ya vyanzo hivi kwa undani zaidi:
Bacterial Pneumonia

Wagonjwa wengi wa pneumonia hushambuliwa na bacteria aitwaye Streptococcus pneumoniae. Watu wanaougua kwa muda mrefu ugonjwa wa obstructive pulmonary disease (COPD) au wale wanaotumia pombe kwa wingi hupata pneumonia kutokana na bacteria waitwao Klebsiella pneumoniae na Hemophilus influenzae. Baadhi ya wagonjwa wengine hupata ugonjwa huu
kutokana na bacteria aitwaye Mycoplasma pneumoniae.

Maji yasiyo salama yakinywewa au kutumika ndani ya viyoyozi husababisha pneumonia kutokana na bacteria aitwaye bacterium Legionella pneumoniae. Kuna aina ya pneumonia, pneumocystis carinii pneumonia, ambayo hushambulia mapafu yote mawili inayotokana na mwili kuwa na upungufu wa kinga unaotokana na magonjwa ya kansa au UKIMWI au kutibiwa rheumatoid arthritis na baadhi ya dawa.
Viral Pneumonia

Hii ni pneumonia inayotokana na virusi na ambayo haisikii tiba za antibiotics. Baadhi ya virusi wa aini hii ni Adenoviruses, rhinovirus, influenza virus (flu), respiratory syncytial virus (RSV), na parainfluenza virus.
Fungal Pneumonia
Aina hii ya pneumonia husababishwa na fangasi wa aina za histoplasmosis, coccidiomycosis, blastomycosis, aspergillosis, na cryptococcosis.

Nosocomial Pneumonia
Viumbe wadogo walioishi kwenye mazingira ya antibiotics kwa muda mrefu hujijengea uwezo wa kuhimili dawa hizo na pindi wakiingia katika mapafu husababisha nosocomial pneumonia. Bacteria wa aina hii hupatikana kwenye majumba ya kuuguzia wagonjwa na katika hospitali.

Mazingira Yanayosababisha Pneumonia

Mazingira au hali zifuatazo zinaweza kusababbisha ugonjwa pneumonia:
Moshi

Unywaji wa pombe wa kukithiri
Magonjwa kama chronic obstructive pulmonary disease (COPD), emphysema, pumu, au UKIMWI.
Umri pungufu ya mwaka mmoja au zaidi ya miaka 65.

Kuwa na kinga ndogo za mwili Utumiaji wa dawa za magonjwa, gastroesophageal reflux disease (GERD).

Kushambuliwa na kifua na mafua Kuwa na lishe duni Kulazwa kwenye hospitali kwenye kitenge cha uangalizi maalumu (Intensive care unit).

Kuwezepo kwenye mazingira ya kemikali za aina fulani au uchafuzi wa hewa.

Kuwa mwenye asili ya Alaska au koo fulani za kimarekani Kuwa nanmatatizo yanayoruhusu chakula kutoka tumboni kuingia kwenye mapafu
Dalili Za Pneumonia

Pneumonia inayotokana na bacteria huonyesha dalili mapema zaidi kuliko ile inayotokana na virusi. Watu wengi wanaopata ugonjwa huu huanza kwa kushikwa na kifua au mafua, kisha kupata homa kali inayoambatana na kikohozi chenye kutoa makohozi. Pamoja na kwamba dalili za pneumonia zinaweza kuwa za aina tofauti kulingana na chanzo chache, wagonjwa wengi huona dalili zifuatazo:

. Kukohoa
. Makohozi ya rangi ya kahawia au kijani
. Homa
. Kuhema kwaharaka na kukosa pumzi
. Kutetemeka
. Maumivu kifuani hasa unapovuta pumzi
. Mapigo ya moyo kwenda mbio
. Uchovu na udhaifu wa mwili
. Kichefuchefu na kutapika
. Kuharisha
. Kutokwa jasho
. Kichwa kuuma
. Maumivu ya misuli
. Kuchanganyikiwa
Tiba Ya Pneumonia

Tiba itakayotolewa kwa mgonjwa wa pneumonia itategemea aina ya pneumonia aliyo nayo na hali aliyonayo mgonjwa. Pneumonia inayotokana na bacteria hutibiwa na antibiotics wakati pneumonia zinazotokana na virusi hutibiwa kwa kumpa mgonjwa muda wa kupumzika na kumpa vinywaji kwa wingi. Pneumonia zinazotokana na fangasi hutibiwa na dawa za kutibu fangasi.
Dawa nyingine hutolewa ili kumsaidia mgonjwa kupunguza homa, kuondoa maumivu ya kichwa, kuondoa mafua na kikohozi. Ni muhimu sana kwa mgonjwa wa pneumonia kupata muda wa kupumzika na kupata usingizi. Mgonjwa hutakiwa kutumia
vinywaji kwa wingi sana.

Mgonjwa hulazwa hospitali pale hali yake inapokuwa mbaya au pale inapobainika kuwa ana upungufu wa kinga za mwili. Kwenye hospitali mgonjwa atapewa antibiotics kupitia mishipa ya damu na wakati mwingine kupewa msaada wa kupumua kupitia mitungi ya oksijeni.
By Welfare


Clink here to view video


No comments

Powered by Blogger.