Header Ads

IZZO BIZNESS-HAKUNA KITU KITAKACHOIYUMBISHA “THE AMAZING”



kundi hilo limejipanga kukabiliana na changamoto ambazo zimekuwa zikiyakabili baadhi ya makundi mengine ya muziki hapa nchini.

Staa huyo na rapper ambaye ameshirikiana na muimbaji, Abela kuunda kundi hilo, amesema kabla ya kuunda kundi hilo walika chini na kuangalia namna ambavyo wataweza kukabiliana na matatizo.

“The Amaizing tumejipanga kupambana na changamoto zote, mpaka kuja au kufikia maamuzi ya kuungana na kuanzisha kundi tayari tumeshasomana tabia, yaani sisi tuna mengi ambayo tuliyaangalia, kwahiyo naweza sema tupo vizuri tunaomba Mungu atusimamie tu,” amesema Izzo
Rapa huyo amesema, muziki kwa sasa umebadilika na kuwafanya wasanii kuacha kutegemea show pekee.

“Kwa sasa ukifanya muziki mzuri utaona matunda ya muziki wako kwa sababu sasa hivi wasanii hatutegemei shows tu, watu wanapata deal kubwa za kupiga show za mkampuni, endorsement na mambo mengine. Kwahiyo mimi naona kuna mashavu mengi sana kwenye muziki kama ukiandaa kazi nzuri,”


No comments

Powered by Blogger.