Header Ads

Matokeo ya Fibroids (complications)

MATOKEO YA FIBROIDS ( COMPLICATIONS)
Zifutazo ni yaweza au yana husiana na vimbe hizi, ingawa kuna vyanzo lukuki za matokeo tajwa hapo chini, hizo ni;
-Maumivu makali wakati wa uja uzito au wati wa kawaida na kuona kiuno kizito
-Mimba kutoka mara kwa Mara, hasa baada ya wiki 12+ ya mimba
-Mimba kutunga nje ya mji wa mimba
-Chupa kupasuka kabla ya labor
- Kupata labor au kuzaa kabla ya wakati wake
-Kuzaa watoto wasio kua vizuri au wenye uzito mdogo kutokana na kukosa nafasi ya kukua vema na kukosa nafasi kutokana na vimbe
-Kuvuja damu kabla ya wiki ya kuzaa ( APH) kutokana na msukumo wa uvimbe kwa Kondo la mimba( abruptio placenta)
-Mtoto kukaa mkao tofauti ndani ya mji wa mimba na kusumbua katika kuzaa
-Pia ni hatari kuhitaji kuzaa kwa operation
-Hatari ya kuvuja damu baada ya kuzaa( PPH)
-Kuna uwezekano mdogo pia wa vimbe hizo chini ya 3% ya uwezekano wa kuwa saratani ( Leiomyosarcoma)

NAMNA YA KUGUNDUA UGONJWA HUO
Vitu 3 muhimu Daktari atahitaji kujua ugonjwa huu
1. Historia au malalamiko kutoka kwa mgonjwa na mnyumbuo wa malalamiko na dalili za mgonjwa

2. Uchunguzi wa kitabibu( Physical examination), daktari anamfanyia uchunguzi mgonjwa kitabibu kwa system zote kulingana atakavyoona
mahitaji

3. Vipimo; Vipimo kama Ultrasound, Hysteroscopy au MRI nk kadiri ya matokeo ya uchunguzi wa awali na dalili za mgonjwa

MATIBABU
Kuwa Fibroid pekee hakumaanishi kuhitaji matibabu, bali huwekwa katika uangalizi maana hupotea baada ya mwanamke kukoma kuona hedhi.
Ikiwa kuna dalili tajwa au mwanamke tashindwa kushika mimba basi kuna njia za kukabiliana na vimbe hizo, kulingana na protocol za kidaktari na hali, umri au zinginezo za Mgonjwa. Kwa kutaja tu ni kama ifuatavyo
- Dawa za kupunguza vimbe hizo ( Medical therapy)
-Upasuaji ( Surgery)
- Na kiradiolojia kwa kuziba mishipa ya damu ambayo vimbe hupata damu kupitia yenyewe ( Interventional Radiology)

No comments

Powered by Blogger.